Harufu ya binadamu ndio huvutia viini vya Malaria


Mbu wanaoambukiza Malaria huvutiwa zaidi na harufu ya mwili wa binadamu kuliko wadudu wengine, kwa mujibu wa utafiti.

Watafiti waliochapisha matokeo ya utafiti wao katika jarida la Plos One, wanaamini kuwa Mbu wanaobeba viini vinavyosababisha Malaria, huwa na uwezo mkubwa wa kunusa.

Daktari James Logan, kutoka chuo cha mafunzo ya fya mjini London, anasema kuwa moja ya mambo ambayo humshangaza ni ambavyo viini vinakuwa na akili nyingi.

Anasema kuwa viini vinaonekana kuwa na akili nyingi kiasi cha kuwa mbele kwa fikira kuliko hata wanasayansi.

Miguu yenye kunuka

Katika kufanya utafiti wao, wanasayanyi waliwaambukiza Mmbu na viini hatari vya Plasmodium falciparum.

Waliwaweka Mmbu hao katika mkebe pamoja na soksi ilyoikuwa inavunda na ambayo ilikuwa imevaliwa kwa masaa ishirini. Mmbu hao walijazana kwenye soksi hiyo

Wanasayansi hao walifanya utafiti huo na Mmbu ambao walikuwa hawana viini hivyo.

Waligundua kuwa Mmbu waliokuwa na viini waliweza kuvutiwa zaidi na soski zilizokuwa na uvundo.

Wanasayansi wanaamini kuwa Mmbu waliokuwa na viini wanakuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kunusa kwa sababu viini ndivyo vinawawezesha kunusa zaidi.

Kwa Mmbu, binadamu anakuwa rahisi kushambulia kwa sababu ya harufu ya mwili wake na kisha viini hivyo ninavamia damu yake kuhakikisha kuwa vinaendelea kuzaana.

Watafiti hao sasa watafanya utafiti wa miaka mitatu kutaka kujua ni vipi viini vina uwezo wa kufanya hivyo.

Daktari Logan , anasema kuwa ikiwa wataweza kujua viini vinavyosababisha Malaria, itawasaidia kupambana na ugonjwa wa Malaria.

Kulingana na takwimu za hivi karibuni, shirika la afya duniani linasema kuwa mnamo mwaka 2012, takriban watu milioni 219 waliugua Malaria huku wengine 660,000 wakiripotiwa kufariki kutokana na ugonjwa huo.

Afrika ndilo bara lenye visa vingi vya watu kuugua Malaria na asilimia tisini ya vifo vinavyotokana na Malaria hutokea barani humo.

DIAMOND ATOBOA KWA NINI KIWEMBE!

                                                   Diamond
                                               Diamond  na Wema
                                                  Diamond na Penny
                                                   Diamond na Joketi
KWA mara ya kwanza nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond' ameacha gumzo London, Uingereza baada ya kueleza sababu za kwa nini ni kiwembe?

Akifunguka katika mahojiano maalum wiki iliyopita na Kipindi cha Sporah Show cha runingani alipokuwa kwenye ziara ya kimuziki nchini humo, Diamond alizungumza ishu kibao za kimapenzi hasa juu ya msururu wa wanawake ambao tayari ametoka nao.
ASISITIZA ANASUBIRI MTOTO
Kabla ya yote, staa huyo alisisitiza kuwa muda si mrefu anatarajia kupata mtoto kutoka kwa mpenzi wake wa sasa, Peniel Mungilwa ‘Penny’ akimaanisha kuwa ni mjamzito, kinyume na msichana huyo ambaye hivi karibuni alimshangaa Diamond kueneza habari hizo.
KWA NINI ANAPENDA KUBADILISHA WANAWAKE?
Diamond: Mimi ni binadamu kama binadamu wengine wa kawaida. Nampenda mwanamke anayenipenda na kuniheshimu. Ikitokea mikwaruzano huwa mimi nakaa pembeni, natafuta sehemu nyingine. Wakati mwingine mimi ndiye huwa naachwa.
KWA NINI MSURURU NDANI YA KIPINDI CHA MIAKA MITATU?
Diamond: Nikiwa na mtu nikiachana naye naonekana nina matatizo kwa sababu wakati mwingine nakuwa na wanawake wenye majina. Siwezi kukaa bila uhusiano na nakuwa wazi kwa sababu lazima itajulikana tu na kuandikwa kwenye magazeti. Kuna kipindi nilikaa miezi sita bila kufanya kitu chochote (mh!). Lakini nikianza (uhusiano), nikihama naonekana msumbufu.
KWA NINI MASTAA, TENA MARAFIKI?
Diamond: Huwa sitoki, nakuwa nyumbani tu, nakaa na mama yangu (Sanura Kassim ‘Sandra’) nampikia. Nikitoka nakwenda kwenye shoo au studio. Huko ndiko nakutana nao (mastaa wa kike).
ALIMPATAJE JOKATE (MWEGELO)?
Diamond: Alikuwa anazindua nguo zake (Kidoti) akaniomba nikapite nazo kwenye onesho la mavazi, nikapita nazo jukwaani. Baada ya hapo na mimi nilimuomba nifanye naye video ya wimbo wangu (Mawazo), ndiyo ikatokea kama hivyo.
NINI KILIMVUTIA KWA PENNY?
Diamond: Kwanza mimi nilimjua Penny kabla ya Wema (Sepetu), alikuwa mshikaji wangu. Ni mwanamke mzuri, wa kileo, ana akili adabu na heshima. Anampenda mama yangu na familia yangu ‘coz’ na mimi nampenda mama yangu (sifa ambazo kwa mujibu wake Wema alizikosa).
KWA NINI ALIMREKODI WEMA?
Diamond: Kila binadamu anajiona yupo sawa na anaonewa. Sipendi kuongea, nitazungumza vibaya. Mapenzi yanaumiza na mimi naumia pia lakini watu wanadhani mimi ndiye muumizaji. Unamwambia mtu kwa nini una mwanaume mwingine.
Anakuzuga sijui ni pedeshee anampa pesa. Mara unamwona na mwanaume mwingine. Mimi siyo maskini lakini sasa mara unamwona na brazameni mwingine ‘then’ washkaji wanakwambia. Wewe unajifanya kuziba masikio mara unasikia ana mwanaume mwingine. Lakini ikafika wakati nikajikuta naumia sana kwenye mapenzi.
Kama ukisikiliza ule wimbo wa Kesho ni kweli kabisa. Mimi nikakaa pembeni hadi nilipompata huyu wa sasa (Penny).
Nakumbuka (Wema) alinipigia simu akadai mimi ndiye nasema anataka turudiane. Nilikuwa kwenye gari, nikamuuliza anataka nini?
Wakati huo nilishafika nyumbani kwa baby wangu. Nikamwonesha ona sasa, anasema mimi ndiyo nataka nirudiane naye, anatangazia watu hadi saluni kuwa nataka kurudiana naye na kujidai kwenye vyombo vya habari kuwa ananipenda. Kumbe ana wengine (ving’asti) kama ishirini anawahonga (mistari ya wimbo wake wa Nataka Kulewa).
Nilimpa baby wangu akamwambia kistaarabu tuache tulale. Sasa kuna mtu wetu wa karibu ndiye aliyehusika kusambaza ile sauti.
SEMA UKWELI, ULILALA NA UWOYA?
Diamond: (kicheko) Ningeanzia wapi? Unajua mimi ni simba kwa hiyo nikionekana na swala inajulikana lazima nimle hata kama tumeenda sehemu tu kuzungumza ishu za kazi.
KWA NINI WANAWAKE AU ENZI ZILE HAKUWA NA ‘CHANSI’ SASA AMEPATA?
Diamond: Ukimuelimisha mwanamke mmoja umeelimisha ulimwengu mzima. Nawapenda sana, wanajaa tele kwenye shoo zangu. Kilichotokea kwa Wema ilibidi tu sikuwa na jinsi.
ANATAKA MWANAMKE WA AINA GANI?
Diamond: Ukimuuliza mwanamke aliyewahi kuwa na mimi atakwambia najua mapenzi, najua kupetipeti, najua kubembeleza, najua kujifanya mjinga. Narudia tena, awe mzuri, wa kileo, mwenye akili, anayejiheshimu, ampende mama yangu kama mimi ninavyompenda mama yangu.
KWA NINI KIWEMBE?
Uchunguzi uliofanywa na Ijumaa ulibaini kuwa chanzo cha staa huyo aliyetokea Tandale, Dar kuitwa kiwembe ni kutokana na tabia yake ya kubadilisha wanawake kama nguo.
Baadhi ya aliowahi kuripotiwa akidaiwa kutoka nao ni Rehema Fabian (Miss Kiswahili 2009), Jacqueline Wolper (msanii wa filamu), Upendo Moshi ‘Pendo’ (Mshiriki wa Maisha Plus) na  Natasha (Video Queen wa Bongo Fleva).
Wengine ni Wema (mwigizaji), Jokate (mwigizaji), Aunt Ezekiel (mwigizaji), Najma (msanii wa Bongo Fleva), Penny (mtangazaji DTV), Irene Uwoya (mwigizaji) na wengineo.
chanzo:globalpublishers

Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Hii imetoka kwenye hotuba ya kambi ya upinzani. Sehemu hii inaonyesha ubadhirifu wa fedha kwenye wizara iliyoko chini ya Dr John Pombe Magufuli.

Mheshimiwa Spika, baada ya fedha hizi kupunguzwa kiasi cha shilingi bilioni 95 na kupelekwa wizara ya uchukuzi zilibakia kiasi cha shilingi bilioni 252.975 katika kifungu hiki, leo tumelazimika kulikumbusha Bunge kuhusiana na suala hili kwani kwa mujibu wa ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ya mwaka husika wa fedha kuhusiana na kifungu hiki alisema, naomba kunukuu “malipo ya madeni ya mwaka wa nyuma yaliyolipwa kwa fedha za 2011/2012 kwa kutumia jina la mradi usio halisi Tshs. 252,975,000,000.


Miradi katika wizara ilipewa namba 4168 kwa ajili ya kupitisha malipo ya madeni ya miaka ya nyuma kwa miradi inayotekelezwa na TANROADS. Namba hii sio halisi” (chanzo: taarifa ya CAG uk.160,fungu 98)


Mheshimiwa Spika, fedha hizi “zilizopotea”au “kulipwa kifungu hewa” ni sawa na fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya barabara ifuatazo kwa mwaka huu wa fedha 2013/2014;

i. Barabara
ya Usagara-Geita-Kyamyorwa
(KM 422)


ii. Barabara
ya Kigoma-Kidahwe-Uvinza-
Kaliua-Tabora (KM 443)


iii. Barabara
ya Nangurukuru-Mbwemkulu
(KM 95)


iv. Barabara
ya Sumbawanga-Matai-Kasanga
Port (KM 112)


v. Barabara
ya Manyoni-Itigi-Tabora (KM264)


vi. Barabara
ya Tabora-Ipole-Konga-Mpanda
(KM 359)


vii. Barabara
ya Kidatu-Ifakara-Lupilo-Malinyi-
Londo-Lumecha/Songea(KM-396)


viii. Kuondoa
msongamano barabara za Dar
(KM-102.15)


Aidha, ni sawa na kusema kuwa barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 316.218 imepotea kwa kutumia mahesabu ya wizara ya ujenzi kuwa kilomita moja ya lami inajengwa kwa kiasi cha shilingi milioni mia nane (800,000,000), hii ni sawa na kusema kuwa barabara ya kutoka Manyoni-Itigi-Tabora (KM 264) Changanya na barabara ya kutoka Chunya – Makongorosi (KM 43) na Barabara ya Tangi Bovu –Goba (KM 9), zimepotea kutokana na ufisadi huu.

Chanzo: Hotuba ya kambi rasmi ya upinzani bungeni

Soma hapa zaidi>>> Jamii Forums

"Siku zote Maisha ndivyo Yalivyo Unapokaribia Mafanikio Ndipo Unapokata Tamaa..."


MATOKEO YA KIDATO CHA NNE KUTANGAZWA WIKI HII HABARI KAMILI IKO HAPA


Matokeo mapya ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012 yanatarajia kutangazwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi siku yeyote wiki hii.

Kutangazwa upya kwa matokeo hayo kunafuatia uamuzi uliochukuliwa na serikali hivi karibuni kufuta wa matokeo hayo ili yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011.

Habari ambazo NIPASHE imezipata jana na kuthibitishwa na viongozi wandamizi wa wizara hiyo, kazi ya kufanya marekebisho ya matokeo hayo imeshakamilika na yatatangazwa wiki hii. 

“Kazi ya kuandaa matokeo imekwishakamilika sababu ni kazi inayofanywa na watu watatu kwa kutumia kompyuta,” alisema ofisa mmoja ambaye alisema taarifa rasmi zitatolewa na Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.

Dk. Kawambwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk. Joyce Ndalichako, walipotafutwa kueleza suala hilo jana, simu zao zilikuwa zikiita bila kupokelewa.
Hata Hivyo, Afisa Habari wa Necta, John Nchimbi, alisema mchakato wa kuandaa matokeo hayo unaendelea na kwamba yatatangazwa muda wowote.
Mei 3, mwaka huu serikali ilitangaza kufuta matokeo hayo na kuamua yaandaliwe upya.


Uamuzi huo wa Serikali ambao ulitangazwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, kwamba umetokana na matokeo mabaya ya mitihani huo yaliyosababisha zaidi ya asilimia 60 ya wanafunzi kupata sifuri. 

Kutokana na matokeo hayo, Serikali iliunda Tume inayoongozwa na Profesa Sifuni Mchome kuchunguza matokeo hayo ili kupata ufumbuzi wa kudumu. 

Katika mtihani wa mwaka 2012, wanafunzi 367,756 walifanya mtihani huo na waliofaulu ni 126,847. Waliofaulu kwa kwa madaraja ya kwanza hadi la tatu ni 23,520 sawa na asilimia 6.4 na daraja la nne ni 103,327 sawa na asilimia 28.1, huku 240,909 ambao ni asilimia 65.5 wakipata daraja sifuri.


CHANZO: NIPASHE

Ngono zembe ilivyokithiri TZ katika barabara ya kuelekea Zambia

makahaba-ngono-zembe

Licha ya kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya Ukimwi, Mkoa wa Mbeya bado unatajwa kuwa eneo lililokithiri kwa vitendo vya ngono bila kuwa na tahadhari (ngono zembe).

Sababu kubwa ya hali hiyo inaelezwa kuwa ni kuwepo kwa maegesho ya malori ya mizigo yanayoelekea Zambia huku madereva wake wakitajwa kuwa wateja wakubwa wa ngono.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Mwananchi Jumamosi katika maeneo yanayotajwa kwa biashara ya ngono yaani..Read More

Source: Mwananchi

Wananchi Mkoani Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi.

Meneja wa Benki ya NMB kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Lucresia Makirie akimkabidhi pikipiki tatu

Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage

Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio Julius Kaijage akimkabidhi pikipiki mbili na matairi 4 ya gari pamoja na mabati mkuu wa mkoa wa Mbeya Abas Kandoro vifaa hivyo vyote vimetoka kwa wadau wa ulinzi mkoani hapa




Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiongea na wadau mbali mbali kwenye hafla fupi ya kupokea misaada toka kwa wadau wa ulinzi mkoani hapa

Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage amesema Askari wa Jeshi la Polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha analiwezesha kwa hali na mali.

Meneja wa Benki ya NMB kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Lucresia Makirie amesema benki yake imetoa msaada Pikipiki tatu kusaidia jeshi hilo ili zisaidie katika ulinzi shirikishi katika mkoa wa Mbeya


Kamanada wa Polisi Mkoani Mbeya Diwani Athumani amewapongeza wadau mbalimbali waliojitokeza kulisaidia jeshi hilo ambapo amewahahakikishia wananchi wa mkoa huu kuwa kwa sasa mkoa wa mbeya upo katika mazingira salama kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wananchi na jeshi hilo .













Picha ya pamoja
BAADHI ya Wananchi Mkoani Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi Mkoani hapa kwa kuendelea kusambaratisha na kumaliza kabisa mtandao wa ujambazi kutokana na majambazi wengi  kukamatwa na wengine kuawa.
  
Pongezi hizo zimekuja Siku moja baada ya Jeshi hilo kuwauwa watu watano wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika majibizano ya kurushiana risasi kati ya Askari na majambazi hayo katika tukio lililotokea katika kijiji cha Garijembe Wilaya ya Mbeya.
  
Katika kuhakikisha Jeshi hilo linaendelea  kufanya kazi katika mazingira mazuri na kwa mafanikio  na kuunga mkono juhudi zao, Wadau mbali mbali  leo  wamejitokeza kulichangia jeshi hilo katika Hafla iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoani hapa.
  
Hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro Jumla ya Shilingi Milioni 28 zilipatikana vikiwemo vifaa mbali mbali.
  
Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage amesema Askari wa Jeshi la Polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha analiwezesha kwa hali na mali.
  
Katika Hafla hiyo Jumla ya Pikipiki tano zilinunuliwa ambapo kati ya hizo Tatu zimetolewa na Benki ya Nmb kwa thamani ya Shilingi Milion 5.4, wakati kamati ikinunua pikipiki Mbili kwa Thamani ya Shilingi Milioni Moja na Laki Nane.
  
Mbali na michango hiyo pia Wakala wa Majengo mkoa wa Mbeya (TBA) imetoa mabati 22 ya Geji 28 yenye thamani ya Shilingi 460,000/=, pia kamati ya Mafanikio imenunua Matairi nane yenye thamani ya Shilingi Milioni 3,020,000/=,pamoja na mafuta kwa ajili ya magari ambayo ni Lita 360 kwa Mwaka zilizoahidiwa na kampuni ya G4S.
  
Mbali na pongezi hizo Wananchi hao wamemshauri Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani mbali na kupambana na uhalifu katika Mkoa wa Mbeya na kuwasisitiza watu wanaofanya shughuli zisizokuwa na uhalali kuacha mara moja au kuhama Mkoa pia wapendekeza kufanya ziara za kushtukiza katika Vituo vidogo vya Polisi.

Kwa upande wake Kamanada wa Polisi Mkoani hapa Diwani Athumani amewapongeza wadau mbalimbali waliojitokeza kulisaidia jeshi hilo ambapo amewahahakikishia wananchi wa mkoa huu kuwa kwa sasa mkoa wa mbeya upo katika mazingira salama kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wananchi na jeshi hilo .

Na Mbeya yetu

HUYU ndo KIJANA ATAKAYE NYONGWA RASMI LEO ASUBUHI!!

Photo: Please share, along with links to the petition.


JK AOMBEA AMANI NA MAASKOFU, ATEMBELEA WAFIWA NA MAJERUHI WA BOMU ARUSHA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mke wake Mama Salma Kikwete wanajiunga na maaskofu wa makanisa mbalimbali katika kuombea amani Tanzania alipokwenda nyumbani kwa Askofu Mkuu wa Katoliki Jimbo la Arusha Archbishop Josephat Lebulu (mwenye kanzu nyeupe) kabla ya kwenda kuhani misiba ya watu watatu waliofariki katika mlipuko wa bomu jijini humo Jumapili iliyopita. Pia alitembelea majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Mtakatifu Elizabeth na ya Mount Meru ambako aliwapa pole majeruhi 31 kati ya 64 waliolazwa hadi sasa.
source:issamichuzi (17)

Baada Ya Kiongozi Wa CLOUDS FM Kuamuru Kutopigwa Kwa BONGO FLAVA Siku Nzima Ya Jana ... Haya Ndio Yaliyojiri Online ...

Kupitia mitandao tofauti ya kijamii, baadhi ya watu maarufu wameonekana wakiandika mawazo yao tofauti juu ya uamuzi alioutoa Bw. Ruge Mutahaba wa kutopiga nyimbo za Bongo Flava siku nzima ya jana katika kituo cha radio cha Clouds FM...
Check baadhi ya posts za baadhi ya wasanii na watu maarufu kuhusiana na tamko hilo hapa chini ...




Bw. Ruge Mtahaba alitamka hayo wakati alipokuwa akifanyiwa mahojiano katika kipindi asubuhi cha Power BreakFast wakati alipokuwa akiongelea ishu nzima kuhusu yeye na Mwanamuziki Lady Jaydee ...
#GongaMx

MKE WA HAMMER Q BAADA YA KUPOKEA KIPONDO KUTOKA KWA MMEWE, HIKI NDO ALICHOKIANDIKA FB KUHUSU WAO KUPATANA


Kitu mapenzi jamani hakuna asiyekijua na moyo ukipenda vigumu kuuzuiaa, mnaambiwa msiingilie wala kushadadia ugomvi wa wawili wanaoongea wakiwa uc***i maana watapatana tu alafu mtaumbuka, basi hiki ndicho kilichotokea kwa Hammer Q na mkewe bibie Salha, pamoja na kupewa kipigo cha haja na mumewe hadi kumpelekea kushonwa nyuzi kadhaa mwilini mwake lakini hiki ndicho alichoandika bibie huyu SALHA muke halali wa HAMMER Q katika account yake ya facebook, WAMBEA MPOOOO!!! MLOKUWA MNASHABIKIA AACHANE NA MUMEWE!! EHEHEEIIYAAAA!!! MNAUMIAJE SASA..!!



Matatizo ameumbiwa binaadam na binaadam ndie anaeyakuza matatizo Kwa binadam mwenzake Na anadiriki kuinyima furaha na amanai nafsi ya mwenzake yote hii ni 7Bu ya roho mbaya. Kuna binadam Wengine Hufurahia kuona binadam mwenzake anapata matatizo Bila ya kukumbuka kuwa matatizo ni kama rizki leo kwa mwenzako kesho kwako,wengine ni watu wazima Ila wamekosa fikra na upeo lkn wamejaaliwa mvi na umri Tu hawana ubinadam.kuna watu wamefurahi baada ya matatizo yangu na mume wangu wengine wameandaa sherehe wengine wanadiriki kutuma sms kwangu eti kwamba hapo bado na tutazidi kuwavuruga, na sms nying nying zenye mafumbo ...dah poleni sana wenye roho nyeusi mulizopewa nyakati za usiku zenye nyota za kichawi ila mungu ndo kiboko yenu 7bu mungu hafananishwii. Kauli ya mwisho ni inayotoka moyoni mwangu na itakayoendelea kutoka mpaka mwisho wa pumzi yangu Mbali na maneno mengi yaliokwisha semwa sehem mbalimbali na kuandikwa lkn mimi ndo muamuzi wa mwisho .nina umri mdogo lkn mungu ameniumba na hekma na busara (asante mungu) na km muliweza kuyaongelea wakati wa matatizo pia kumbukeni kuyaongelea na wakati wa furaha pia kumbuka mungu amemuumba binadam..Lkn Na binadam amejikabizi maslahi ya uovu ktk mdomo wake kuongea anachotaka ilimradi aonekane bora bila ya kumkumbuka aliemuumbA. juwa kwamba binadam Alie buni dawa ndie aliebuni ugonjwa na aliebuni silaha ndie mchochezi wa vita ilimradi afanye biashara zake anenepe na familia yake..namshkuru mungu naendelea vizuri tna sana nawashkuru mlokuja kuniangalia nawashkuru munaonijali mpakamda huu nawashkuru pia mulionishauri mazuri na mabaya nyote ni muhimu kwangu kiroho safi nitaendelea kuwa -_--
Salha wa hammer Full stop nampenda mume wangu 
Usiku mwema




KILA LA KHEIR SALHA HOPE MTAISHI VYEMA NA MUMEO NA WENYE VIJIBA NA KUTAKA KUWAARIBIA WATASHINDWA KWA NGUVU YA ALLAH SUBHANNAH

KAMA HUJACHUKUA FOMU, BOMBA FM RADIO YATANGAZA AJIRA MOJA.


Kituo cha Bomba Fm 104.OMHz Mbeya kimetangaza ajira moja katika kituo hicho, ambapo mmoja kati ya watu watakaokuwa wakiwania nafasi hiyo ya ajira watashindana moja kwa moja kupitia vipindi viwili.
 
Mshindi wa mashindano atapatikana kwa ushirikiano mkubwa kati yake na wasilikilizaji ambao ndio watakuwa majaji wakuu……

VIGEZO vya mshiriki:-
1. Awe na umri wa kuanzia miaka 18.
2. Awe raia wa Tanzania.
3. Awe na elimu ya kuanzia Kidato cha nne.
4. Awe hana mkataba wowote na kampuni yoyote ile.
5. Awe hajawahi kufungwa jela au kushitakiwa na kosa lolote.
6. Awe na akili timamu.

*Mwisho wa uchukuaji Fomu ni June 15, 2013.

*Fomu ya ushiriki ni shilingi 10,000/= tu ya Kitanzania   

*Kama upo nje ya Mkoa wa Mbeya maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia simu ya mkononi.+255764 240 440 na vilevile unaweza kulipia gharama ya Fomu kupitia namba hiyo hiyo.

Lauryn Hill gets 3 months for failing to pay taxes

FILE - This April 15, 2011 file photo shows singer Lauryn Hill performing during the 12th Coachella Valley Music and Arts Festival in Indio, Calif. Hill is facing sentencing Monday, May 6, 2013 in New Jersey on federal tax charges. Hill pleaded guilty last year to not paying federal taxes on $1.8 million earned from 2005 to 2007. A judge two weeks ago said Hill had paid only about $50,000 of more than $500,000 she owes. Hill said she has signed a recording contract with Sony that will help her pay her taxes. Citing the legal deadline, she made a song available on iTunes over the weekend. She faces up to a year in prison on each of three counts. Her attorney is seeking probation for her. (AP Photo/Spencer Weiner, file)
Associated Press/Spencer Weiner, file - FILE - This April 15, 2011 file photo shows singer Lauryn Hill performing during the 12th Coachella Valley Music and Arts Festival in Indio, Calif. Hill is facing sentencing …more 


NEWARK, N.J. (AP) — Grammy-winning singer Lauryn Hill stood in federal court Monday and compared her experience in the music business to the slavery her ancestors endured before a judge sentenced her to three months in prison for failing to pay about $1 million in taxes over the past decade.

"I am a child of former slaves who had a system imposed on them," Hill said before U.S. Magistrate Madeline Cox Arleo. "I had an economic system imposed on me."

Hill, who started singing with the Fugees as a teenager in the 1990s before releasing her multiplatinum 1998 album "The Miseducation of Lauryn Hill," pleaded guilty last year to failing to pay taxes on more than $1.8 million earned from 2005 to 2007. Monday's sentencing also took into account unpaid state and federal taxes in 2008 and 2009 that brought the total earnings to about $2.3 million.

Despite having paid more than $900,000 in the past several days, Hill still owes interest and penalties, the U.S. attorney's office said.

In a forceful but controlled statement to the judge punctuated by occasional raps with her first on the podium, Hill described how she failed to pay taxes during a period when she'd dropped out of the music business to protect herself and her children, who now number six.

She said the treatment she received while she was in the entertainment business led to her decision to leave it.

"There were veiled threats, there was blacklisting," she said, without giving specifics. "I was told, 'That's how it goes, it comes with the territory.' I came to be perceived as a cash cow and not a person. When people capitalize on a persona, they forget there is a person in there."

In addition to serving three months in prison, Hill must pay a $60,000 fine. After she is released from prison, she will be under parole supervision for a year, the first three months of which will be spent under home confinement.

The 37-year-old South Orange resident had faced a maximum sentence of one year each on three counts of failing to file taxes. Her attorney had sought probation, arguing that Hill's charitable works, her family circumstances and the fact she paid back the taxes she owed should merit consideration.

Assistant U.S. Attorney Sandra Moser acknowledged Hill's creative talent and work on behalf of impoverished children but called Hill's explanation for her actions "a parade of excuses centering around her feeling put upon" that don't exempt her from her responsibilities.

"She wasn't interested in all those years in paying what she owed," Moser told the judge.
At the time of her arrest last year, Hill wrote a criticism rejecting pop culture's "climate of hostility, false entitlement, manipulation, racial prejudice, sexism and ageism."

"Over-commercialization and its resulting restrictions and limitations can be very damaging and distorting to the inherent nature of the individual," Hill wrote. "I did not deliberately abandon my fans, nor did I deliberately abandon any responsibilities, but I did however put my safety, health and freedom and the freedom, safety and health of my family first over all other material concerns! I also embraced my right to resist a system intentionally opposing my right to whole and integral survival."

Hill is to report to prison by July 8. It's not clear where she'll serve her sentence. She didn't comment after the sentencing.

She said in a recent post online that she has signed a recording contract with Sony.
"She is looking forward to putting her case behind her and getting back to her music and creating again," attorney Nathan Hochman said.

FLORA MBASHA KUINGIA KWENYE SIASA.

Show ya Diamond Uingereza yawa na dosari, Mchezaji wa Chelsea Adam Nditi aiponda.

Mtanzania ambaye kwa sasa ni raia wa Uingereza na anayechezea klabu ya Chelsea, Adam Nditi ameiponda show ya Diamond mjini Reading nchini humo na kudai ilikuwa ni aibu tupu.
“Diamond jana manyago aibu tupu waswahili lazima tubadilike it’s embarrassing,” ametweet.


“Hajafanya jambo lolote ila shoo ilikuwa very unprofessional kwenye tangazo walisema inaanza saa 3 usiku jamaa amefika saa 1 asubuhi.”


“Jukwaa lilikuwa ovyo kama vile watu hawajalipa kumuuona mmoja Wa wasani wanaotamba bongo nyimbo zilikuwa zinapigwa redioni alikuwa haimbi.”

Kwa sasa Diamond yupo ziarani nchini Uingereza.

Kamati ya kuisaidia Taifa Stars na huu ndiyo muda wenu

Timu ya Taifa ya soka ‘Taifa Stars’ ipo kwenye mashindano ya kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Brazil mwaka 2014.

Katika Afrika, Tanzania (Taifa Stars) imepangwa kundi C kati ya makundi 10. Kundi C linajumuisha timu za Ivory Coast, Morocco, na Gambia.

Kwa sasa katika Kundi C, Taifa Stars inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi sita, nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba, Morocco ina pointi mbili na Gambia ina pointi moja.

Kwa hali ilivyo hivi sasa, Taifa Stars ipo katika nafasi nzuri ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2014, lakini ili Tanzania ifuzu fainali hizo inatakiwa ishinde mechi zote tatu zilizobaki na kuongoza kundi C na baadaye iingie katika timu kumi bora ili baadaye zishindane na zipatikane timu tano kutoka Afrika ambazo zitafuzu kwenda Brazil katika Fainali za Kombe la Dunia 2014.

Kutokana na Taifa Stars kufanya vizuri katika hatua ya makundi na kubakisha mechi tatu dhidi ya Morocco, Ivory Coast na Gambia, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara ameunda Kamati ya Saidia Taifa Stars Ishinde.

Wajumbe wa Kamati hiyo inayoongozwa na Mbunge wa Singida Mjini, Mohammed Dewji, ni Teddy Mapunda, Dk Ramadhani Dau, Dioniz Malinzi, Asji Shabir, George Kavishe, Mohammed Raza (Mbunge), Leodger Tenga, Joseph Kusaga, Kapteni John Komba na Zitto Kabwe (Mbunge).

Kamati hiyo baada ya kuteuliwa ilitakiwa na waziri kuanza kazi mara moja na iliambiwa hadidu za rejea zitakazowaongoza kutekeleza majukumu yao watazipata Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Pia, Serikali iliahidi kutoa ushirikiano utakaohitajika kwa kamati hiyo ambayo inaundwa na wadau mbalimbali wa soka ili ifanye kazi iliyopewa vizuri na kuiwezesha Taifa Stars kushinda mechi zote zilizobaki. Sisi tunaitakia kila la kheri Kamati hiyo ya kuisadia Taifa Stars ishinde kwani tunaamini imeundwa kwa dhamira ya dhati na katika muda mwafaka wa kuisaidia Taifa Stars.

Tunasema hivyo kwa sababu hivi sasa Ligi Kuu ya Tanzania Bara inaelekea ukingoni mwezi huu, ambapo kamati hiyo kwa kushirikiana na viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na benchi la ufundi la Taifa Stars wanatakiwa kuhakikisha wachezaji watakaoteuliwa kuunda kikosi cha Taifa Stars wanaingia kambini mapema kwa ajili ya maandalizi ya mechi zake za kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwezi Juni.

Taifa Stars haijawahi kucheza Fainali za Kombe la Dunia zaidi ya kuishia hatua za awali za kufuzu, lakini kama mikakati ikiandaliwa kikamilifu, nafasi hiyo ipo.

Sisi tunaamini kuwa Taifa Stars ikipata ushindi katika mechi dhidi ya Morocco na Ivory Coast, ushindi huo utafufua na kutia chachu nafasi ya Tanzania kufika mbali katika mashindano hayo ya kufuzu.

Kinachotakiwa kufanywa hivi sasa ni kamati hiyo ya kuisaidia Taifa Stars ishinde kutafuta fedha za kutosha, ambapo zikiunganishwa na fedha za wadhamini wa Taifa Stars basi Taifa Stars itapata maandalizi mazuri ikiwamo kuweka kambi nje ya nchi.

Pia tunaamini kocha wa Taifa Stars atachagua wachezaji wenye uwezo, uzalendo wa hali ya juu, umoja na kujenga lengo moja la kutafuta ushindi.

Tunaamini Kamati ya kuisadia Taifa Stars kushinda itafanya kazi zake kwa bidii na kufuta dhana ambayo imejengeka katika jamii kuwa kamati hiyo haina umuhimu.Text inakuja hapa.

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. CHIMBUKO LETU - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger